Ruanda-Urundi
From Wikipedia
Ruanda-Urundi ni jina la zamani kwa ajili ya nchi za Rwanda na Burundi. Zote mbili zilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani hadi 1916. Baadaye zilikabidhiwa na Shirikisho la Mataifa kama eneo la kuhifadhiwa kwa Ubelgiji.
Ubelgiji ilitawala nchi zote mbili kama eneo moja la "Ruanda - Urundi". Wakati wa mwisho wa utawala wa kikoloni sehemu zote mbili ziliachana tena na kuingia katika uhuru kama nchi mbili za Rwanda na Burundi.