Okapi
From Wikipedia
Okapi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Okapi
|
||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
|
Okapi (Okapia johnstoni) ni mamalia wa familia ya twiga. Umbo lake hufanana na farasi ina michoro miguuni kama punda milia lakini haina uhusiano naye ni aina ya twiga.
Okapi ni myama iliyojulikana na wenyeji wa maeneo yao tu hadi 1901. Imeaminika kupatikana tu katika misitu ya Ituri lakini mwaka 2006 dalili zimepatikana ya kwamba iko pia kwenye misitu ya hifadhi ya kitaifa ya Kongo ya Virunga. Kwenye misitu ya Ituri kuna hifadhi ya okapi yenye 14,000 km².
Shingo ni fupi kuliko twiga lakini ina ulimi mrefu sana wa kujipatia majani unaomwezesha kusafisha masikio yake yeye mwenyewe. Duma ina pembe mbili fupi kichwani.
Ukubwa wa okapi ni hadi 2.5 m kichwani na hadi 2 m mabegani. Anafikia uzito kati ya 200 hadi 250 kg. Anakula majani ya miti pamoja na manyasi, matunda na uyoga.
[edit] Viungo vya nje
[edit] Picha
Okapi kwenye bustani ya wanyama ya Bristol (Uingereza) |
Okapi wa dume akionyesha ulimi kwenye bustani ya wanyama ya Bristol (Uingereza) |