Hidekeli
From Wikipedia
Mto wa Hidekeli | |
---|---|
|
|
Chanzo | Milima ya Taurus katika Uturuki |
Mdomo | Ghuba ya Uajemi kwenye Shatt al Arab |
Nchi | Uturuki, Syria, Iraq |
Urefu | 1,850 km |
Kimo cha chanzo | ?? m |
Mkondo | 1500 m³/s (wastani) |
Eneo la beseni | 258,000 km² |
Mto Hidekeli (Kiajemi: tigr, kar.: دجلة, dijla, kituruki/Kikurdi: dicle, Kiaramu: deqlath, Kiebrania: חידקל hidekel) ni mto wa Asia ya magharibi. Pamoja na Frati ni mto mkubwa wa Mesopotamia.
Contents |
[edit] Etimolojia
Jina la Kiswahili lina asili yake katika Kiebrania cha Biblia kinachohifadhi jina la kale kabisa cha Kiakkadi linaloendelea pia katika maumbo la jina hili kwa Kiarabu, Kituruki, Kikurdi na Kiaramu.
[edit] Mwendo
Hidekel ina chanzo chake katika milima ya Uturuki ya Mashariki. Kwa kilomita chache inapita eneo la Syria halafu inaingia katika Iraq. Baada ya kuvuka milima ya Kurdistan inapita mji wa Mossul na kuingia katika tambarare ya Mesopotamia. Inafika Baghdad na kuendelea katika Iraq ya kusini hadi kuungana na mto Frati katika Shatt al Arab ambayo ni mpaka kati ya Iraq na Uajemi. Mdomo uko katika pembe la Ghuba ya Uajemi.
[edit] Mito ya kando
Mito ya kando muhimu ni:
- katika Uturuki: mto Batman
- katika Iraq: mto Zab
- katika Uajemi: mto Karun
[edit] Malambo
Uturuki na pia Iraq zimejenga malambo mbalimbali hasa kwa kusudi la maji ya kumwagilia maeneo makavu. Wataalamu wanaona hatari ya kuhatarisha ekolojia ya mto kwa njia hii. Lakini mazingira ya sehemu kubwa ya mwendo wa mto ni kavu sana na mahitaji ya maji ni makubwa. Faida ya malambo imekuwa mwisho wa mafuriko yaliyotokea zamani hasa katika mwezi wa Aprili wakati wa kuyeyuka kwa theluji milimani.
[edit] Malambo katika Uturuki
- lambo la Kralkızı
- lambo la Dicle
- lambo la Cizre
- lambo la Ilısu
- lambo la Garzan
- lambo la Kayser
- lambo la Silvan
[edit] Malambo katika Syria
Syria inapanga kujenga vituo vya kuvuta maji kutoka Hidekeli
[edit] Malambo katika Iraq
- lambo la Mossoul
- lambo la Samara
- lambo la Kut
- lambo la Makhul