Brazil
From Wikipedia
|
|||||
Wito la taifa: Ordem e Progresso (Kireno kwa "Utaratibu na Maendeleo") |
|||||
Wimbo wa taifa: Ouviram do Ipiranga as margens plácidas ("Kando ntulivu za Ipiranga zilisikia...") |
|||||
![]() |
|||||
Mji mkuu | Brasilia |
||||
Mji mkubwa nchini | Sao Paulo | ||||
Lugha rasmi | Kireno | ||||
Serikali
Rais
|
Shirikisho la Jamhuri Luiz Inacio Lula da Silva |
||||
Uhuru Ilitangazwa Ilitambuliwa Jamhuri |
7 Septemba 1822 29 Agosti 1825 15 Novemba 1889 |
||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
8,514,877 km² (ya 5) 0.65 |
||||
Idadi ya watu - 2005 kadirio - 2000 sensa - Msongamano wa watu |
186,405,000 (ya 5) 169,799,170 22/km² (ya 182) |
||||
Fedha | Real (BRL ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC-2 to -5 (Official: -3)) (UTC) |
||||
Intaneti TLD | .br | ||||
Kodi ya simu | +55 |
Brazil ni nchi kubwa ya Amerika ya Kusini na pia nchi yenye wakazi wengi kushinda nchi zote za bara hii. Eneo lake ni karibu nusu ya bara yote. Imepakana na Uruguay, Argentina, Paraguay, Bolivia, Peru, Kolombia, Venezuela, Guyana, Surinam na eneo la Guyana ya Kifaransa. Brazil ina pwani ndefu ya Atlantiki.
Wakazi walio wengi hutumia lugha ya Kireno lakini kuna lugha nyingi kwa sababu ya vikundi vya wenyeji asilia (Waindios) na wahamiaji kutoka pande zote za dunia.
Mji mkuu ni Brasilia mji uliopangwa na kujengwa kati ya 1957 na 1960. Mji mkubwa ni Sao Paulo.
Contents |
[edit] Jiografia
Misitu mipana ya dunia inapatikana Brazil katika beseni ya mto Amazonas. Misitu hii inafunika takriban 40% ya eneo la nchi. Idadi kubwa ya wakazi hukalia maeneo katibu na pwani ya Atlantiki. Kitovu cha kilimo ni nyanda za "cerado" au savana katika magharibi ya kati ya Brazil.
[edit] Miji muhimu
Jiji kubwa ni São Paulo linalofikia pamoja na mitaa ya jirani kwenye idadi ya wakazi milioni 20.5 Mio.
Majiji ya kufuata ni Rio de Janeiro (wakazi mio. 11.4), Belo Horizonte (wakazi mio. 4.3), Porto Alegre (wakazi mio. 4), Recife (wakazi mio. 3.6), Fortaleza na Salvador da Bahia (wakazi mio. 11.4 kila jiji) na Brasilia (wakazi mio. 2.2).
São Paulo ni jiji kubwa kabisa linalokua haraka sana. Ni moyo wa kiuchumi wa Brazil mwenye viwanda vingi.
Rio de Janeiro ilikuwa mji mkuu wa nchi hadi kuanzishwa kwa Brasilia. Imejulikana koto duniani kutokana na uzuri wa mazingira yake na sherehe ya Kanivali . Ina pia viwanda muhimu ni kitovu cha utamaduni.
Mji mkuu wa Brasilia ulijengwa kama ishara ya umoja wa nchi katika miaka mitatu pekee.
Jumla ya asilimia 70 za wakazi hukalia miji mikubwa.
[edit] Milima
Mlima mkubwa ni Pico da Neblina (3,014 m juu ya UB) pamoja na Pico 31 de Março (2,992 m) ulio karibu naye kwenye mpaka wa Brazil, Venezuela na Guyana.
Mlima mkubwa wa kusini ni Pico da Bandeira (2.891 m) .
Mlima unaojulikana zaidi si mkubwa lakini uko ndani ya mji wa Rio de Janeiro ni Corcovado mwenye 710 m. Juu yake kuna sanamu ya Yesu Kristo ambayo ni ishara ya mji.
[edit] Mito muhimu
Brazil ina mto mkubwa na mrefu wa dunia ambayo ni Amazonas mwenye urefu wa takriban 7000 km. Tawimito yake muhimu ni Río Purús, Rio Negro na Rio Tapajós. Katika mashariki kuna mto Iguaçu mwenye maporomoko ya Iguaçu ambayo ni makubwa duniani.
Parana (3.998 km) ni mto mrefu duniani baada ya Amazonas. Inalisha kituo kikubwa cha nishati ya maji duniani cha Itaipú.
Lagoa dos Patos karibu na Porto Alegre ni wangwa kubwa la Brazil lenye 10.000 km².
Ipiranga si mto mkubwa hata kama jina lake linapatikaka katika wimbo wa taifa.
[edit] Visiwa
Brazil ina visiwa vichache vidogo katika Atlantiki kama vile
- Penedos de São Pedro e São Paulo (miamba ya Mt. Petro na Mt. Paulo)
- Kisiwa cha matumbawe cha Rocas
- Fernando de Noronha
- Trindade e Martim Vaz
Visiwa hivi ni sehemu ya mgongo kati wa Atlantiki; hali halisi ni vilele vya milima inayoanza kwenye msingi wa bahari.
Kisiwa kikubwa cha Brazil hakipo baharini lakini katika mto Amazonas ni Marajó chenye eneo la 48.000 km² (kubwa kushinda eneo la Uswisi).
[edit] Hali ya hewa
Hali ya hewa ni ya kitropiki isipokuwa katika kusini.
Beseni ya Amazonas ina mvua nyingi. Kwenye milima ya kusini usimbishaji unaweza kutokea kama theluji.
[edit] Historia
Brazil imekaliwa na watu tangu miaka 10,000. Waindio waliingia kutoka kaskazini. Hakuna taarifa za kimaandishi lakini akiolojia imeweza kufumbua makazi mbalimbali ya wenyeji asilia.
[edit] Ukoloni
Brazil ilikuwa koloni ya Ureno kutokana na mkataba wa Tordesillas ambamo Hispania na Ureno zilipatana tar. 5 Septemba 1494 ugawaji wa dunia kati yao baada ya fumbuzi za Kolumbus.
Mreno wa kwanza aliyefika mwambao wa Brazil tar. 22 Aprili 1500 alikuwa Pedro Alvares Cabral. Makazi ya kwanza ya Wareno ni mji wa São Vicente mwaka 1532. Mji mkuu wa kwanza ulikuwa bandari ya Salvador da Bahia tangu 1549. Wareno walianzisha kilimo cha miwa wakiwalazimisha Waindio wenyeji kuwafanyia kazi. Walianza kuingia ndani ya bara wakitafuta watumwa kwa ajili ya mashamba na dhahabu.
[edit] Hali ya Waindio
Wenyeji walipungua haraka kwa sababu ya kuambukizwa na magonjwa ya kigeni wakikosa kinga dhidi yao, halafu kutokana kutendewa vibaya kama watumwa mashambani. Wareno walianza kutafuta wafanyakazi penginepo kwa kuchukua watumwa kutoka Afrika.
[edit] Mapadre Wayesu
Katika hali hii wamisionari wakristo wa Chama cha Yesu walisimama upande wa Waindio. Walijipatia tamko rasmi la Papa wa Roma ya kuwa Waindio ndio wanadamu kamili hawafai kutendewa kinyama. Wakibatizwa na kuwa Wakristo walitakiwa kukubaliwa kama raia wa Kireno yeyote – amri ambayo mara nyingi haikukubaliwa na wavindaji wa watumwa na wenye mashamba.
Mapadre wa Chama cha Yesu walianzisha „reduciones“ yaani vijiji na miji kwa ajili ya Waindio walipoishi chini ya ulinzi wao na kutetewa dhidi ya wavindaji wa watumwa. Katika makazi hao Waindio walifundishwa shule kwa lugha za kienyeji na Kireno na kupata mafunzo wa ufundi mbalimbali. Kwa njia hii mapadre hawa walitawala maeneo makubwa ndani ya bara.
Hali ilisababisha hasira ya wanasiasa Wareno walioendelea kuwapinga hadi Ureno penyewe. Mwaka 1767 mapadre wa chama cha Yesu walilazimishwa kuondoka katia Ureno na koloni zake zote.
[edit] Upanuzi wa Brazil
Karne ya 17 na ya 18 iliona kuanzishwa kwa miji mizuri kwa sababu dhahabu na almasi zilifumbuliwa katika misitu ya beseni ya Amazonas. Misafara ya kutafuta hazina hizi zilipanua eneo la Brazil kuelekea magharibi. Mji Mkuu ulihamishwa kwenda Rio de Janeiro mwaka 1763.
[edit] Uhuru 1822
Uhuru wa Brazil ulisababishwa na siasa za Ulaya. Mwaka 1807 Ureno ilivamiwa na Ufaransa ya Napoleon Bonaparte. Mfalme wa Ureno João VI alikimbia Brazil, Rio de Janeiro ikawa mji mkuu wa dola la Ureno. Mfalme aliporudi Ureno mwaka 1821 alimwachia mtoto wake Pedro utawala wa Brazil. Mwaka 1822 Pedro aliyeona mabadiliko ya kimapinduzi katika koloni za Hispana kote Amerika ya Kusini aliamua kutangaza uhuru wa Brazil akiwa mwenyewe mfalme kwa cheo cha Kaisari.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Brazil" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Brazil kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |